Hayawi hayawi hatimae yanatarajiwa kuwa!
Ule mchakato wa
kumtangaza Sr. Bernadetha Mbawala kuwa mwenyeheri unatarajiwa kufungwa
tarehe 14 January, 2013 ikiwa ni miezi kumi tu badala ya miaka miwili
kama ilivyo ada.
Habari hii njema ilitolewa na
mwakilishi wa Baba Mtakatifu- Benedicto XVI Braza Cruz aliyefika
nchini hivi karibuni kuja kutathimini mchakato mzima.
Kwa
kawaida mchakato wa kumtangaza Mtumishi wa Mungu kuwa Mwenyeheri, una
ngazi kuu mbili; Mosi ni ngazi ya jimbo na pili ni ngazi kuu ya
Vatikano. Ngazi ya jimbo kwa mfano watoa shuhuda zinazokubalika hutakiwa
kuwa 30 lakini kwa sista Bernadeta wamefika 52.
"Nimeridhika
na kazi nzuri ambayo imefanyika katika kumtangaza sista Bernadeta
Mbawala katika ngazi ya jimbo" alisema Braza Cruz.
Ingawa
mchakato umefikia hatua nzuri kijimbo, hatua ya pili ni kubwa sana na
gharama ni kubwa. Tunawasihi marafiki wote wa Sr. Bernadeta kuendelea
kumuomba Mungu kupitia maombezi yake na mpeleke shuhuda zenu katika
kamati ya mchakato jimbo kuu la Songea. Pia tunawahimiza kuendelea
kuchangia mchakato huu kifedha kwa kutumia akaunti iliyowekwa hapa
kwenye blogu au kwa kuwasiliana na mkuu wa kamati ya fedha Fr. Francis
Shawa 0769 845995
Taarifa hii imeletwa na Albano Midelo-
Kamati ya habari, mchakato wa Sr. Bernadeta
This blog is about the life of a Benedictine nun of St Agnes Chipole-Songea Tanzania who is on her way to sainthood.The blog supports the cause for her beatification by defusing the information so that the faithful can ask for her intercession and offer their moral and financial support to the Archdiocese of Songea to effect the process
SR BERNADETA FUND
Kindly assist the Archidiocese of Songea by contributing to the beatification process of Sr. Bernadeta Mbawala through their CRDB account no. 0152085128521, account name:SR. BERNADETA FUND