Je umeshawahi kusaidiwa shida yeyote kama ugonjwa, masomo, kazi n.k? kupitia maombi ya Sr. Bernadeta Mbawala? unaweza kushare nasi? Please do!
Vicenza-Marie
This blog is about the life of a Benedictine nun of St Agnes Chipole-Songea Tanzania who is on her way to sainthood.The blog supports the cause for her beatification by defusing the information so that the faithful can ask for her intercession and offer their moral and financial support to the Archdiocese of Songea to effect the process
SR BERNADETA FUND
Kindly assist the Archidiocese of Songea by contributing to the beatification process of Sr. Bernadeta Mbawala through their CRDB account no. 0152085128521, account name:SR. BERNADETA FUND
Tuesday, April 24, 2012
Monday, April 23, 2012
MASALIA YA MWILI WA SR BERNADETA YAPATIKANA
Maaskofu wa majimbo nane ya metropolitani ya Songea wakishuhudia ufukuaji wa mwili wa Sr Bernadeta Mbawala |
Mwili wa Sr Bernadeta ulifunguliwa mnamo tarehe 24 January, 2012 mbele ya maaskofu wa metropolitani ya Songea ambayo inahusisha majimbo nane ambayo ni Songea, Njombe, Mbinga, Mbeya, Iringa,Tunduru Masasi,Lindi na Mtwara.
Siku ya ufukuzi wa Kaburi hilo watu wengi walivutika kuja kuona kilichomo kani moja, mni jambo geni lakini pili wengi walipatwa na shahuku ya kujua nini kinaweza kitakachoweza kupaatikana kwa mtu aliyekufa miaka hamsini(50) iliyopita.
Sr Bernadeta akinyanyuliwa kuelekea madhabahu ya bwana, kabuli li tupu sasa |
“Mwanzoni tulidhani hakutakuwa na kitu baada ya kukuta mchwa wengi lakini tulipochimba zaidi tlishangaa kuiona mifupa yake, punje za rozari na msalaba” Alisema Fr Francis Shawa ambaye yuko kwenye kamati ya mchakato huu.
Kwa sasa masalia hayo yamehifadhiwa katika kikanisa cha Askofu Mkuu mwashamu Norbert Mtega wa jimbo kuu katoliki la Songea. Kwa sasa utaratibu unaofanyika katika Kanisa Kuu la Kiaskofu Songea wa kujenga mahali rasmi ili kuweka masalia ndani ya Kanisa.
Mifupa na msalaba pia vilipatikana |
Maaskofu wakishuhudia masalia ya Sr. Bernadeta |
Ukiwa umehifadhiwa katika jeneza, mwili wa Sr. Bernadeta ukiingizwa katika kanisa kuu la Mt. Matias Mulumba- Songea |
Hivi karibuni rafiki Vicenza-Marie alipata nafasi ya kuongea na Baba Askofu Norbert Mtega Kurasini Dar eslaam na katika maongezi hayo baba pia aliongelea swala la uhifadhi wa masalia. “Itapasa pia masalia ya Mtumishi wa Mungu yaliyoko Chipole yajengewe mahali maalum pa kuyaweka ndani ya Kanisa, kwani ni muhimu na ni lazima kisheria kufanya hivyo ili kutoa fursa kwa waamini na watu wengine kusali mbele ya Masalia ya Mtumishi wa Mungu na kufanya hija yao huko”
Katika madhabahu ya bwana |
Vilevile baba alisema ya kwamba “Pamoja na sehemu hizo mbili yalipohifadhiwa masalia hayo, itabidi tutengeneze upya kaburi lake pale Peramiho, ili hapo pia pawe ni mahali maalum pa hija kwa watu binafsi wanaotaka kuhiji. Hivyo, hija zitaweza kufanyika: Songea, Chipole, Peramiho na Luwawazi-Likuyufusi, mahali alipozaliwa,”
Saturday, April 21, 2012
Sr Bernadeta Mbawala; Badiliko la jina la blogu
Dear Marafiki,
Kwakuwa blogu hii imeamua kutoa sapoti kwa mchakato wa Sr Bernadeta basi tumeona vyema tukibadili na jina ila kuwarahisishia watafutaji wa blogu hii.
Asanteni sana
Vicenza-Marie
Kwakuwa blogu hii imeamua kutoa sapoti kwa mchakato wa Sr Bernadeta basi tumeona vyema tukibadili na jina ila kuwarahisishia watafutaji wa blogu hii.
Asanteni sana
Vicenza-Marie
Friday, April 20, 2012
MAPENZI MAKUU KWA MAMA BIKIRA MARIA
Dear Marafiki
Sr Bernadeta akisali katika kipango (Grotto) ya mama Bikira Maria, Peramiho. |
Leo tunaangalia kwa kifupi uhusiano wa watakatifu; wao kwa wao. Unadhani kitu gani wanashabihiana? Katika kupitia vitabu mbalimbali vya maisha ya watakatifu, nimegundua vitu vingi ambavyo wanashabihiana. Mfano wa maeneo/ viyu hivyo ni pamoja na Mapenzi yao na imani thabiti kwa Ekaristi takatifu,imani kwa mama Bikira Maria na mateso;kuyapenda na kuyavumilia kwa saburi wakiyatolea kwa nia mbalimbali.
Sr Bernadeta alikuwa na mapenzi makubwa kwayo pia. Mapenzi kwa Ekaristi na kwa mama Bikira Maria
Sr Bernadeta Mbawala;tumuombe, tumtangaze, kwa sifa na utukufu wa Mungu!
Vicenza-Marie!
Thursday, April 19, 2012
CHANGIA MCHAKATO WA Sr. BENADETA KUPITIA MFUKO WA BENADETA WA JIMBO KUU KATOLIKI SONGEA
Mchakato wa safari ya uenye heri ya rafiki yetu Sr Benadeta Mbawala ni ghali mno. Tunaombwa kumuongezea Mwashamu baba Askofu Mkuu Norbet Mtega nguvu. Wameanzisha mfuko pale jimboni kupitia Bank ya CRDB:
Sr Bernadeta Fund, CRDB Bank, Account number. 0152085128521
Chonde Chonde
"Sr Benadeta Mbawala: Tumtangaze, Tumuombe kwa sifa na utukufu wa Mungu"
Vicenza- Marie
Subscribe to:
Posts (Atom)