Darasa la watoto wakatekisimu |
Dear Marafiki
Alice, Erick and Vicenza- marie wameamua kuwafundisha watoto Katekisimu ya kanisa katoliki.
Sote watatu ni vijana wa jumuiya ya Mt. Francisco wa Asizi, Parokia ya Maria Mtakatifu Kimara Mwisho. Parokia yetu iko barabara ya Morogoro na wote wapitao hapo aidha wakiwa wanaenda au wanatoka mikoani ni lazima wapite hapo. Basi toka ukiwa mbali utaona minara mirefu na paa la kanisa letu zuri. Ingawa parokia yetu inamiaka mitano tu, imekuwa sana sana kutokana na maombezi ya msimamizi wetu mama Maria Mtakatifu, mapadri wetu waklareti (Claretian Fathers) pamoja na waumini wote.
Katika Parokia yetu pia huwa tunaabudu Ekaristi takatifu kwa kukesha kila ijumaa ya kwanza ya mwezi. Pia kila siku milango huwa wazi hadi saa mbili au tatu usiku ili watu waweze kuendesha sala zao binafsi.
Pia tuna grotto kubwa sana ya mama Maria na kwa sasa tunajenga nyumba ya mapadri. Well, kibali kitatoka ndani ya wiki mbili lakini michango bado inaendelea.
Back to Katekisimu klass, basi sisi vijana watatu wa parokia tuliona ni vyema kama tungewafundisha wadogo zetu imani yetu Katoliki ili waweze kukua vyema kama Yesu mwenyewe.
Kiukweli tunaona ni baraka ya pekee kuvifundisha vitoto hivi katekisimu. Vinafurahi kweli hata sisi tunapata furaha kubwa sana moyoni.
Mmoja wa walimu wa Katekisimu Alice Mchomvu akiwasikiliza watoto |
Masomo hayo hufundishwa kila siku ya jumamosi mara tu baada ya jumuiya. Watoto hukusanyika nyumbani kwa Vicenza-marie ambako hufundishwa kisha hupata chai.
Wanajifunza yafuatayo
1. Katekisimu ya kanisa katoliki
2. biblia
3.Maisha ya watakatifu (Pia huangalia sinema mbalimbali za maisha ya watakatifu zilizo katika katuni)
4. Huchora vitu mbalimbali vya kwenye biblia
5. kuimba na
6. Kujifunza nyimbo mbalimbali.
Watoto wa darasa la Katekisimu wakijiandaa kuangalia filamu ya maisha ya Mt. Francisco wa Asizi |
Tunapenda kuwahamasisha vijana wengi mjitolee kuwafundisha wadogo zenu imani yenu Katoliki.
"Najivunia ukatoliki wangu"- Angela Kessy |
"Kwahiyo, yeyote ambae atawafundisha wengine mambo haya ataitwa mdogo katika ufalme wa Mungu, lakini kwa yeyote atakayeyaishi haya na kuwafundisha wengine ipasavyo ataitwa mkuu katika ufalme wa Mungu"
Ndani ya upendo wa kristu,
Vicenza-Marie of the Eucharist