Wanajumuiya tuliungana katika kuadhimisha misa siku hiyo kisha tarehe 28/01/2012 ndipo tulipofanya tafrija fupi nyumbani kwa Vicenza-marie (Mama Mchu...)kule Kimara mwisho.
Basi mambo yalikuwa hivi...
Fr Joseph Mosha na Lilian Mallya wakijipumzisha baada ya kazi nzito ya upishi
"Hapa wakizubaa tu nakimbia na sufuria la pilau" Ndivyo anavyoonekana da Lilian Akiwaza
Tunamshukuru Mungu sana pamoja na Mt. Francis de Sales kwa kuifanikisha sherehe yetu. Sasa tutamuenzi muombezi wetu kimatendo zaidi katika kutayatafuta, kuyatafakari na kuyaishi mapenzi ya Mungu.
Tunawashukuru wooooooooooooote waliofika na wale walioifanikisha sherehe yetu kwa njia moja au nyingine.
Katika upendo wa Kristu,
Vicenza-marie!